MWILI WA DKT. SENGONDO MVUNGI KUWASILI IJUMAA NOVEMBA 15 2013, KINANA AMLILIA
Rais Jakaya Kikwete
akitia saini kitabu cha maombelezo ya kifo cha Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya
Katiba Dkt. Sengondo Mvungi nyumbani kwake Kibamba jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba wakifurahia jambo na Waziri wa Katiba
na Sheria Mathias Chikawe (kushoto), Makamu Mwenyekiti wa Tume Jaji Mkuu
Mstaafu Augustino Ramadhani na Mjumbe wa Tume Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Salim
Ahmed Salim (kulia) walipokutana nyumbani kwa marehemu Dkt. Sengondo Mvungi
Kibamba jijini Dar es Salaam.
(Picha na Tume ya Katiba)
Rais Jakaya Kikwete (katikati) akibadilishana
mawazo na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba (kushoto)
nyumbani kwa marehemu Dkt. Sengondo Mvungi walipokwenda kuipa pole familia.
Kulia ni Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi James Mbatia na Mjumbe wa Tume Waziri Mkuu
Mstaafu Dkt. Salim Ahmed Salim.
Mjumbe wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba Richard Lyimo akimpa pole mke wa marehemu Dkt. Sengondo
Mvungi, Bi. Anna Mvungi wakati Wajumbe wa Tume walipokwenda kumpa pole.
Rais Jakaya Kikwete akimpa
pole mke wa marehemu Dkt. Sengondo Mvungi, Bi. Anna Mvungi alipokwenda kumpa
pole nyumbani kwake Kibamba jijini Dar es Salaam.
wenyekiti wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba wakifurahia jambo na Waziri wa Katiba
na Sheria Mathias Chikawe (kushoto), Makamu Mwenyekiti wa Tume Jaji Mkuu
Mstaafu Augustino Ramadhani na Mjumbe wa Tume Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Salim
Ahmed Salim (kulia) walipokutana nyumbani kwa marehemu Dkt. Sengondo Mvungi
Kibamba jijini Dar es Salaam.
(Picha na Tume ya Katiba)
.............................................................................................................................
Tume ya Mabadiliko ya Katiba inawafahamisha wananchi
kuwa taratibu za kuusafirisha mwili wa Mjumbe wake, Dkt. Sengondo Mvungi aliyefariki
nchini Afrika Kusini zimekamilika na mwili wake unatarajia kuwasili nchini siku
ya Ijumaa, Novemba 15, 2013.
Baada ya kuwasili, mwili huo utahifadhiwa katika
Hospitali ya Jeshi Lugalo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Aidha, siku ya Jumamosi, Novemba 16, 2013 kutafanyika Ibada
ya mazishi katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph jijini Dar es Salaam kuanzia
saa 4:00 asubuhi. Baada ya misa, marehemu ataagwa katika Viwanja vya Karimjee
kuanzia saa 6:30 mchana siku hiyohiyo ya Jumamosi, Novemba 16, 2013.
Aidha, Marehemu Dkt. Mvungi anatarajiwa kusafirishwa siku
ya Jumapili, Novemba 17, 2013 kwenda Kisangara Juu, Wilaya ya Mwanga mkoani
Kilimanjaro kwa ajili ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika siku ya Jumatatu,
Novemba 18, 2013.
Dkt. Mvungi alifariki jana (Jumanne, Novemba 12, 2013)
katika Hospitali ya Millpark jijini Johannesburg
nchini Afrika Kusini alikopelekwa kwa ajili ya uchunguzi na matibabu zaidi akitokea
Kitengo cha Mifupa Muhimbili (MOI) aliokuwa amelazwa baada ya kuvamiwa nyumbani
kwake Kibamba, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam na watu waliomjeruhi
vibaya kichwani usiku wa kuamkia siku ya Jumapili, Novemba 3, 2013.
Wakati
huohuo,
Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wakiongozwa na Mwenyekiti wake Jaji
Joseph Warioba leo (Jumatano, Novemba 13, 2013) wameungana na Mheshimiwa Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kufika nyumbani
kwa marehemu Dkt. Mvungi eneo la Kibamba jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa
pole kwa familia, ndugu na jamaa wa marehemu Dkt. Mvungi.
Mwisho.
Imetolewa na:
Ndg. Assaa A. Rashid,
Katibu,
Tume ya Mabadiliko ya Katiba,
Dar es Salaam
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Katibu
Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Abdulrahaman Kinana
amesikitishwa na taarifa ya kifo Cha Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya
Katiba Dr Sengondo Mvungi kilichotokea Jana katika Hospitali ya
Millpark nchini Afrika ya Kusini.
Kwa
niaba ya Chama Cha Mapinduzi, Katibu Mkuu anawapa pole wanafamilia,
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba na Uongozi
wa Chama Cha NCCR-Mageuzi. Hakika Taifa limepoteza Mtaalamu wa
Sheria, Kiongozi Mzalendo na hodari katika kipindi ambacho mawazo
yake yanahitajika kwa kiasi kikubwa kuliendeleza Taifa hili.
Mwenyezi
Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi.
Imetolewa
na:
KATIBU
WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA
ITIKADI
NA UENEZI
13/11/2013
Habari kwa hisani ya www.francisgodwin.blogspot.com
No comments:
Post a Comment