ADVERT 1

ADVERT 1
Kilio na kimbilio la wanahabari Tanzania

Sunday, November 17, 2013

Babu wa Loliondo atangaza watu kumiminika upya, Apata maono mengine.

millard
Millard Ayo wa Clouds FM Alipokua akifanya mahojiano na Mchungaji Ambilikile Masapila maarufu kama Babu wa Loliondo
Hivi karibuni mtangazaji maarufu Millard Ayo katika kipindi chake cha Ampifaya alifanya mahojiano na Mchungaji Ambilikile Masapila na kuelezea kwa urefu mwanzo wa huduma yake ya kikombe, changamoto, walioiga kutoa vikombe, vipingamizi pamoja na waliokufa, ambao hawakupona hawakufuata masharti ya dawa.
Mwishoni mwa mahojiano Babu wa Loliando akasema kuhusu mafuriko mapya yatakayotokea hivi karibuni huko Samunge, alizungumza hivi
Siwezi kusema moja kwa moja kwamba ni mwezi wa tatu, ingekuwa pengine mpaka sasa tungeanza kupata watu wengi, na inawezekana ikawa mwezi huo wa tatu, au kabla au baada, mimi siwezi kusema moja kwa moja kwasababu kuna vipingamizi vingi tu, ambavyo Mungu anasubiri vitimie ndipo kazi hiyo ianze, Kuna miujiza mingi imeandikwa ndani ya biblia kitabu cha Mwanzo, Zaburi, Ezekiel, Ufunuo yapo maajabu mengi ambayo Mungu ameyaandika hayakutimia katika nchi ya Israel yatatimia hapa, Samunge, kwahiyo mafuriko ya watu watakaokuja si kwa ajili ya kunywa dawa tu lakini ni kwa ajili ya mambo mbali mbali kuja kuona miujiza ya Mungu itakayofanyika
Alipoulizwa ni maajabu gani yatakayofanyika akasema
“Si vizuri, sijamwambia mtu yeyote ba hata hapa kwako sitasema, isipokuwa mimi nimeyaona mengi tu nimeyaona tayari lakini Mungu hajaniambia tangaza napewa (Maono) kila wakati linakuja hili, linakuja hili napewa kila wakati lakini si zaidi ya labda nusu mwaka sasa
Ili kulinganisha habari ndipo mtangazaji Millard Ayo alipomuuliza Mchungaji Onesmo Ndegi ni maajabu gani hayo ya kwenye biblia
Mchungaji akasema “Hakuna muujiza ambao haujatendeka zaidi ya ule muujiza wa unyakuo, miujiza mingine yote iliyotabiliwa ilishatendeka kwa mfano ukisoma muujiza mkubwa sana ambao Mungu aliuzungumza kutoka Mwanzo 3:15 biblia inasema hivi nami nitaweka uadui kati yako na huyu mwanamke na kati ya uzao wako na uzao wake huo utakuponda kichwa na wewe utauponda kisigino, sasa hapa alikuwa anazungumzia juu ya ujio wa Kristo na ushindi wa Kristo dhidi ya nguvu za giza au shetani na ilishatokea na tunaishi katika kipindi hicho, Yesu Kristo alishakuja akazaliwa, na uwezo wake ukadhibitika ushindi dhidi ya shetani ulionekana pale msalabani, kwa hiyo hakuna muujiza mwingine ambao utasema kuanzia mwanzo haujatimia sasa kuna mtu anataka kuutimiliza, hakuna muujiza wa namna hiyo
Babu wa Loliondo alipoulizwa tena ana ushauri gani kwa Serikali juu ya maajabu  hayo makubwa yatakayotokea hivi karibuni akajibu
Nilitaka kusema kwa upande wa Serikali, nitasema ya kwamba Serikali iwe makini kupokea watu watakaokuja maana ni wengi, ni mafuriko kwa hiyo wawe makini”
Hata hivyo babu amewasamehe watu wote waliomsema vibaya “Kisasi ni kwa Bwana” alisema
–Millard Ayo

No comments:

Post a Comment