ADVERT 1

ADVERT 1
Kilio na kimbilio la wanahabari Tanzania

Tuesday, November 12, 2013



Fahamu Utamaduni Mila na Desturi ya Mtanzania

Watanzania wana simulizi za kusisimua kuhusu asili yao.  Hapo zamani za kale, kutokana na uso wa ardhi kutokuwa mgumu, ardhi ilipasuka na kusababisha Bonde la Ufa ambalo linatanda kuanzia kusini mwa Yemen kupitia nchi za Afrika ya Mashariki ikiwemo Tanzania, hadi Ziwa Nyasa na kugawanyika magharibi kati ya Tanzania na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo.  Moja ya sehemu mashuhuri sana katika Bonde hilo ikatokea ndiyo chimbuko la binadamu.  Binadamu wa awali anafanana na nyani na kwamba fuvu lake na nyayo ziligunduliwa na familia ya Leakeys hapo mwaka 1959 na 1979.  Ushahidi huu ambao ni matokeo ya uvumbuzi wa elimukale kuhusu binadamu wa kwanza ulipatikana katika Bonde la Olduvai na Laetoli.  Maeneo hayo yalikuwa baadhi ya makazi ya ukoo safu wa kisasa (homo habilis na homo sapiens), wazee wa kitanzania ambao waliweza kufikiri na kutengeneza vifaa vinavyotokana na mawe.  Mabaki muhimu ya vifaa na mifupa vilivyoachwa na aina ya binadamu, vinakadiriwa kuwa na umri wa miaka milioni moja na sabini na tano elfu.  Aidha, ushahidi kamahuo umechimbuliwa kwenye maeneo ya kihistoria huko Isimila katika Nyanda za Juu za Kusini ambako vifaa vya kale, vijulikanavyo kama shoka vinaweza kuonekana leo.  Michoro kwenye mapango ya Kondoa-Irangi iliyochorwa na babu zetu hao na dalili za shughuli za uhunzi na umwagiliaji maji mashamba ni ushahidi mwingine wa kuwepo kwa dalili za mtu wa kwanza katika Tanzania kwa wakati wa kale.  Ni vyema kusadiki na kukubali kutoka hapo ni kwamba baadhi ya wazao walitawanyika duniani kote na baadaye kurejea Tanzania kujiunga na dada na kaka zao waliobaki hapa nchini.  Hao sasa walirejea kama wapiganaji wakulima, wachungaji walowezi, wavamizi, wakimbizi, wakoloni, wafanyabiashara, wavumbuzi, wamisionari au watafuta watumwa.  Idadi kubwa ya watu hao ndiyo wanaunda jamii ya watanzania wa leo ikiwa ni pamoja na makabila makubwa (asilimia 99) bila kuwajumuisha makundi madogo kutoka  Ulaya na Asia (asilimia 1).  Kutokana na kukosekana kwa hali ya utulivu kama kawaida na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe katika nchi za jirani hivi sasa na hata hapo zamani, Tanzania imekuwa ni mahala pa makimbilio kwa wahamiaji.  Wakimbizi kutoka makutano ya Benini-Benne Africa magharibi, Bahr el Ghazal nchini Sudan na maeneo ya Shunygwaya nchini Kenya wote walihamia Tanzania kati ya karne ya tatu na kumi na tatu.  Hii leo Tanzania bado anapokea na kuwahudumia maelfu ya wakimbizi kutoka Burundi, Rwanda, Somalia na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo.  Hali hii inaleta mgongano mkubwa kwa idadi ya watu nchini, rasilimali na mazingira.  Idadi ya wakimbizi hao inakadiriwa kuwa kati ya 500,000 hadi 1,000,000.  Wakimbizi wamesababisha athari kubwa kwa nchi hii.  Kutokana na mahitaji ya chakula, maji na kuni, karibu vyanzo vyote vya maji na mimea ya asili ya sehemu husika na jirani ya kambi hizo za wakimbizi zimeharibiwa.  Matokeo yake ni  kwamba maeneo hayo yamegeuzwa kuwa maeneo yasiyokuwa na kitu, maeneo yaliyo katika hali ya jangwa.
 
Mauaji, wizi  na aina nyingine za maovu yamefanywa na baadhi ya wakimbizi na hivyo kusababisha usumbufu kwa jamii na kutoweka kwa amani kwa baadhi ya raia wa Tanzania.  serikali ya Tanzania, Umoja wa Nchi za Afrika (OAU), Shirika la Umoja wa Mataifa la kushughulikia  wakimbizi (UNHCR) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Watoto (UNICEF) wanajitahidi kuwarekebisha wakimbizi hao ili wakati muafaka ukifika warejeshwe makwao.
 
Kwa jumuiya ya kimataifa suala la wakimbizi ni eneo lingine ambalo linahitaji msaada zaidi kwa Tanzania ili kuiwezesha kuwasaidia wakimbizi hao kuishi kama binadamu wengine pamoja na kusaidia kuleta amani kwenye nchi zao ili ziweze kuwa mahala pa kuishi.
 

Utamaduni, mila na desturi

Hali ya mvuto wa mfumo ya jamii wa Tanzania ni kivutio kikubwa kwa masuala ya utamaduni, uchumi na utalii.  Hadithi za watu wa kale, ngoma za asilia na aina ya ngoma zinatofautiana kati ya kabila na kabila.  Wanapocheza, Wamakonde kuchezesha viuno vyao kwenda sambamba na ngoma ya “sindimba”, Wazaramo humezwa na maandamano ya “mdundiko”.  Wamaasai huruka kwa mpangilio maalum huko wakitoa  sauti nzito ambazo zinaweza kumwogofya simba dume!  Matumizi ya nyoka hai na kucheza na nyoka wakubwa kama chatu kunakofanywa na Wasukuma wakati wanacheza ngoma ya “Bugobogobo” hakuwezi kusahaulika kwa mgeni.  Kila kabila kati ya  makabila 120 ya Tanzania ina ngoma yake na staili zake za uchezaji ambazo zinapumbaza kwa kukazia macho zinafurahisha na kuvutia kijinsia.
 
Aina mbalimbali ya mavazi pia hutoa mvuto  wa aina yake kwa mgeni.  Wanaume wa Kimasai huvaa vazi ambalo halifuniki mwili wote huku wakitembea na mikuki, virungu na visu vikubwa.  Kwa upande wao, wanawake wa Kimasai hujaza tele shingo zao, mikono, miguu na masikio yao na vitu vya thamani vikiwemo shanga na hadi aina nyingine za madini.  Wanaume wa Kimasai hupakaza miili yao na udongo mwekundu uliochanganywa na mafuta yatokanayo na wanyama na husuka nywele zao.

Wamakonde nao huchonga meno yao na kuchanja nyuso na miili yao taaluma inayotamanisha.  Wamakonde ni wataalam wa kuchonga vinyago vinavyoonyesha matatizo ya binadamu, mapambano, mapenzi, tamaa, wema, ubaya na mshikamano vitu ambavyo vinavutia sana na kuamsha fikra.
 
Wakazi wa pwani na visiwani hupamba mikono, miguu, midomo na kucha kufuatana na tukio shughuli ambayo huleta mvuto mkubwa.
 
Kati ya makabila ya namna ya pekee ni makundi ambayo yanakadiria kutoweka yaishiyo kati ya Tanzania.  Makabila  haya ni ya Wasandawe (wanahusiana na Waethopia) ambao jirani zao ni wa Iraqw gorowa na burungi na Wadzapi ambao pia hujulikana kama Watindiga na Wakangeju na Wahontetot - wanaohusiana na kabila la Khosa la Afrika Kusini ambao huzungumza lugha za “click”.  Wandorobo pia wanazungumza lugha hiyo lakini wameiga zaidi utamaduni wa nje ya mazingira yao.  Watanzania hao ni wa kuhamahama, wachumaji matunda, wawindaji wakusanyaji chakula, na wavuvi waishio katika eneo linalozunguka Ziwa Eyasi ambalo liko kilomita chache kutoka bonde maarufu la Ngorongoro.  Inasemekana kwamba idadi ya watu hawa kwa sasa haifikii 500 wakati mwaka 1965 walikuwa zaidi ya 30,000.

Wito hapa ni kuisaidia Serikali ya Tanzania kuwaokoa watu hao wasifikie ukingo wa kutoweka.  Kwa maana hiyo, maeneo yanayozunguka Ziwa Eyasi ni bora kabisa ya kufanyia utafiti wa kisayansi wa elimu ihusuyo habari za asili na maendeleo ya  binadamu kwa ajili ya kumbukumbu za baadaye.  Kinachojitokeza ni kwamba ni vyema kutambua kuwa huu ni wakati muafaka wa kufanya uchunguzi ama vile watu hao watakuwa wametoweka kabisa.

No comments:

Post a Comment