Fahamu Utamaduni Mila na Desturi ya Mtanzania
Watanzania
wana simulizi za kusisimua kuhusu asili yao.
Hapo zamani za kale, kutokana na uso wa ardhi kutokuwa
mgumu, ardhi ilipasuka na kusababisha Bonde la Ufa ambalo
linatanda kuanzia kusini mwa Yemen kupitia nchi za Afrika ya
Mashariki ikiwemo Tanzania, hadi Ziwa Nyasa na kugawanyika
magharibi kati ya Tanzania na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo.
Moja ya sehemu mashuhuri sana katika Bonde hilo ikatokea
ndiyo chimbuko la binadamu. Binadamu
wa awali anafanana na nyani na kwamba fuvu lake na nyayo
ziligunduliwa na familia ya Leakeys hapo mwaka 1959 na 1979.
Ushahidi huu ambao ni matokeo ya uvumbuzi wa elimukale
kuhusu binadamu wa kwanza ulipatikana katika Bonde la Olduvai na
Laetoli. Maeneo hayo
yalikuwa baadhi ya makazi ya ukoo safu wa kisasa (homo habilis na
homo sapiens), wazee wa kitanzania ambao waliweza kufikiri na
kutengeneza vifaa vinavyotokana na mawe.
Mabaki muhimu ya vifaa na mifupa vilivyoachwa na aina ya
binadamu, vinakadiriwa kuwa na umri wa miaka milioni moja na
sabini na tano elfu. Aidha,
ushahidi kamahuo umechimbuliwa kwenye maeneo ya kihistoria huko
Isimila katika Nyanda za Juu za Kusini ambako vifaa vya kale,
vijulikanavyo kama shoka vinaweza kuonekana leo.
Michoro kwenye mapango ya Kondoa-Irangi iliyochorwa na babu
zetu hao na dalili za shughuli za uhunzi na umwagiliaji maji
mashamba ni ushahidi mwingine wa kuwepo kwa dalili za mtu wa
kwanza katika Tanzania kwa wakati wa kale. Ni vyema kusadiki na kukubali kutoka hapo ni kwamba baadhi ya
wazao walitawanyika duniani kote na baadaye kurejea Tanzania
kujiunga na dada na kaka zao waliobaki hapa nchini.
Hao sasa walirejea kama wapiganaji wakulima, wachungaji
walowezi, wavamizi, wakimbizi, wakoloni, wafanyabiashara,
wavumbuzi, wamisionari au watafuta watumwa.
Idadi kubwa ya watu hao ndiyo wanaunda jamii ya watanzania
wa leo ikiwa ni pamoja na makabila makubwa (asilimia 99) bila
kuwajumuisha makundi madogo kutoka Ulaya na Asia (asilimia 1).
Kutokana na kukosekana kwa hali ya utulivu kama kawaida na
mapigano ya wenyewe kwa wenyewe katika nchi za jirani hivi sasa na
hata hapo zamani, Tanzania imekuwa ni mahala pa makimbilio kwa
wahamiaji. Wakimbizi
kutoka makutano ya Benini-Benne Africa magharibi, Bahr el Ghazal
nchini Sudan na maeneo ya Shunygwaya nchini Kenya wote walihamia
Tanzania kati ya karne ya tatu na kumi na tatu.
Hii leo Tanzania bado anapokea na kuwahudumia maelfu ya
wakimbizi kutoka Burundi, Rwanda, Somalia na Jamhuri ya Demokrasia
ya Kongo. Hali hii
inaleta mgongano mkubwa kwa idadi ya watu nchini, rasilimali na
mazingira. Idadi ya
wakimbizi hao inakadiriwa kuwa kati ya 500,000 hadi 1,000,000.
Wakimbizi wamesababisha athari kubwa kwa nchi hii.
Kutokana na mahitaji ya chakula, maji na kuni, karibu
vyanzo vyote vya maji na mimea ya asili ya sehemu husika na jirani
ya kambi hizo za wakimbizi zimeharibiwa.
Matokeo yake ni kwamba
maeneo hayo yamegeuzwa kuwa maeneo yasiyokuwa na kitu, maeneo
yaliyo katika hali ya jangwa.
Mauaji,
wizi na aina nyingine
za maovu yamefanywa na baadhi ya wakimbizi na hivyo kusababisha
usumbufu kwa jamii na kutoweka kwa amani kwa baadhi ya raia wa
Tanzania. serikali ya Tanzania, Umoja wa Nchi za Afrika (OAU), Shirika
la Umoja wa Mataifa la kushughulikia
wakimbizi (UNHCR) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Watoto
(UNICEF) wanajitahidi kuwarekebisha wakimbizi hao ili wakati
muafaka ukifika warejeshwe makwao.
Kwa
jumuiya ya kimataifa suala la wakimbizi ni eneo lingine ambalo
linahitaji msaada zaidi kwa Tanzania ili kuiwezesha kuwasaidia
wakimbizi hao kuishi kama binadamu wengine pamoja na kusaidia
kuleta amani kwenye nchi zao ili ziweze kuwa mahala pa kuishi.
Utamaduni, mila na desturi
Hali
ya mvuto wa mfumo ya jamii wa Tanzania ni kivutio kikubwa kwa
masuala ya utamaduni, uchumi na utalii.
Hadithi za watu wa kale, ngoma za asilia na aina ya ngoma
zinatofautiana kati ya kabila na kabila.
Wanapocheza, Wamakonde kuchezesha viuno vyao kwenda
sambamba na ngoma ya “sindimba”, Wazaramo humezwa na
maandamano ya “mdundiko”.
Wamaasai huruka kwa mpangilio maalum huko wakitoa
sauti nzito ambazo zinaweza kumwogofya simba dume!
Matumizi ya nyoka hai na kucheza na nyoka wakubwa kama
chatu kunakofanywa na Wasukuma wakati wanacheza ngoma ya
“Bugobogobo” hakuwezi kusahaulika kwa mgeni.
Kila kabila kati ya makabila
120 ya Tanzania ina ngoma yake na staili zake za uchezaji ambazo
zinapumbaza kwa kukazia macho zinafurahisha na kuvutia kijinsia.
Aina
mbalimbali ya mavazi pia hutoa mvuto
wa aina yake kwa mgeni.
Wanaume wa Kimasai huvaa vazi ambalo halifuniki mwili wote
huku wakitembea na mikuki, virungu na visu vikubwa.
Kwa upande wao, wanawake wa Kimasai hujaza tele shingo zao,
mikono, miguu na masikio yao na vitu vya thamani vikiwemo shanga
na hadi aina nyingine za madini.
Wanaume wa Kimasai hupakaza miili yao na udongo mwekundu
uliochanganywa na mafuta yatokanayo na wanyama na husuka nywele
zao.
Wamakonde
nao huchonga meno yao na kuchanja nyuso na miili yao taaluma
inayotamanisha. Wamakonde
ni wataalam wa kuchonga vinyago vinavyoonyesha matatizo ya
binadamu, mapambano, mapenzi, tamaa, wema, ubaya na mshikamano
vitu ambavyo vinavutia sana na kuamsha fikra.
Wakazi
wa pwani na visiwani hupamba mikono, miguu, midomo na kucha
kufuatana na tukio shughuli ambayo huleta mvuto mkubwa.
Kati
ya makabila ya namna ya pekee ni makundi ambayo yanakadiria
kutoweka yaishiyo kati ya Tanzania.
Makabila haya
ni ya Wasandawe (wanahusiana na Waethopia) ambao jirani zao ni wa
Iraqw gorowa na burungi na Wadzapi ambao pia hujulikana kama
Watindiga na Wakangeju na Wahontetot - wanaohusiana na kabila la
Khosa la Afrika Kusini ambao huzungumza lugha za “click”.
Wandorobo pia wanazungumza lugha hiyo lakini wameiga zaidi
utamaduni wa nje ya mazingira yao. Watanzania hao ni wa kuhamahama, wachumaji matunda, wawindaji
wakusanyaji chakula, na wavuvi waishio katika eneo linalozunguka
Ziwa Eyasi ambalo liko kilomita chache kutoka bonde maarufu la
Ngorongoro. Inasemekana
kwamba idadi ya watu hawa kwa sasa haifikii 500 wakati mwaka 1965
walikuwa zaidi ya 30,000.
Wito
hapa ni kuisaidia Serikali ya Tanzania kuwaokoa watu hao wasifikie
ukingo wa kutoweka. Kwa
maana hiyo, maeneo yanayozunguka Ziwa Eyasi ni bora kabisa ya
kufanyia utafiti wa kisayansi wa elimu ihusuyo habari za asili na
maendeleo ya binadamu
kwa ajili ya kumbukumbu za baadaye. Kinachojitokeza ni kwamba ni vyema kutambua kuwa huu ni
wakati muafaka wa kufanya uchunguzi ama vile watu hao watakuwa
wametoweka kabisa.
No comments:
Post a Comment