JIFUNZE JINSI YA KUTENGENEZA JUISI YA MCHANGANYIKO WA MATUNDA
Na; Ugulumo Natharine - Morogoro
KAMA WEWE NI MVIVU KUNYWA MAJI BASI ANZA
KUJIFUNZA KWA KUNYWA KINYWAJI HIKI KILICHOKAMILIKA KISHA POLE POLE
UTAANZA KUYAPENDA MAJI
MAHITAJI
450 grams Nanasi
50 grams Tangawizi fresh osha vizuri menya
1 Carrot,
JINSI YA KUANDAA FUATILIA PICHA NA MAFUNZO HAPO CHINI
Muda wa maandalizi : Dakika 15
Muda wa mapishi : Dakika 15
Idadi ya wanywaji : watu wawili
Tunda la nanasi na karoti vinachangia sana sukari yote ambayo juisi
inatakiwa iwenayo. Tangawizi inaweka uwiano sawa wa ladha kati ya nanasi
na karoti, kama sio mpenzi wa tangawizi sio lazima kuitumia, lakini kama
ni mpenzi wa nanasi au karoti unaweza kuzidisha kimojawapo ili upate ladha halisi ya unachokipenda.
Tangawizi: Inategemea na ubora wa tangawizi, unaweza
kuhitaji nyingi zaidi au wastani cha msingi uweze kupata harufu mwanana
katika juisi yako.
Menya vizuri nanasi yako kisha katakata vipande vidogo kama inavyoonekana
Chukua vipande vya nanasi, karoti na tangawizi kisha saga kwenye blenda.
Saga vizuri kisha chuja vizuri kwa chujio iliyo safi.
Baada ya kuchuja kama haijachujika vizuri, basi ongeza maji baridi na
safi kiasi tu kisha chuja tena na kisha utapata juisi safi kabisa laini
Kwa sasa ipo tayari waweza kumpatia mnywaji ikiwa ya baridi. Kinywaji safi kabisa
kwa majira ya joto yanayokuja hivi karibuni. Waandalie familia yako waweze kufurahia na nakuwajengea tabia ya
kuzoea kunywa maji.
No comments:
Post a Comment