ADVERT 1

ADVERT 1
Kilio na kimbilio la wanahabari Tanzania

Tuesday, November 12, 2013


 JIFUNZE JINSI YA KUTENGENEZA JUISI YA MCHANGANYIKO WA MATUNDA

Na; Ugulumo Natharine - Morogoro
KAMA WEWE NI MVIVU KUNYWA MAJI BASI ANZA KUJIFUNZA KWA KUNYWA KINYWAJI HIKI KILICHOKAMILIKA KISHA POLE POLE UTAANZA KUYAPENDA MAJI
MAHITAJI
450 grams Nanasi
 50 grams Tangawizi fresh osha vizuri menya
1 Carrot, 
 
JINSI YA KUANDAA FUATILIA PICHA NA MAFUNZO HAPO CHINI
Muda wa maandalizi : Dakika 15 
Muda wa mapishi : Dakika 15
Idadi ya wanywaji : watu wawili
Tunda la nanasi na karoti vinachangia sana sukari yote ambayo juisi inatakiwa iwenayo. Tangawizi inaweka uwiano sawa wa ladha kati ya nanasi na karoti, kama sio mpenzi wa tangawizi sio lazima kuitumia, lakini kama ni mpenzi wa nanasi au karoti unaweza kuzidisha  kimojawapo ili upate ladha halisi ya unachokipenda.
Tangawizi: Inategemea na ubora wa tangawizi, unaweza kuhitaji nyingi zaidi au wastani cha msingi uweze kupata harufu mwanana katika juisi yako.

Menya vizuri nanasi yako kisha katakata vipande vidogo kama inavyoonekana 

Chukua vipande vya nanasi, karoti na tangawizi kisha saga kwenye blenda.

Saga vizuri kisha chuja vizuri kwa chujio iliyo safi.

Baada ya kuchuja kama haijachujika vizuri, basi ongeza maji baridi na safi kiasi tu kisha chuja tena na kisha utapata juisi safi kabisa laini

Kwa sasa ipo tayari waweza kumpatia mnywaji ikiwa ya baridi. Kinywaji safi kabisa kwa majira ya joto yanayokuja hivi karibuni. Waandalie familia yako waweze kufurahia na nakuwajengea tabia ya kuzoea kunywa maji.

No comments:

Post a Comment