ADVERT 1

ADVERT 1
Kilio na kimbilio la wanahabari Tanzania

Tuesday, November 12, 2013

MSIBA MKUBWA TANZANIA DR MVUNGI AFARIKI DUNIA

Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dkt. Edmund Mvungi (katikati) akibadilishana mawazo na Makamishina wa Tume ya Pamoja ya Fedha (JFC), Dkt. Juma Ngasongwa (kulia) na Mhe. Othman Masoud, ambaye ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) mara baada ya JFC kuwasilisha maoni yao kuhusu Katiba Mpya wakati wa mkutano wao uliofanyika katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam.

Mvungi Wafanyakazi -
Jumatano Januari 9, 2013: Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk. Edmund Mvungi (katikati) akizungumza na Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA) waliofika katika Ofisi za Makao Makuu ya Tume Jijini Dar es Salaam leo kuwasilisha maoni yao kuhusu Katiba Mpya.

Na Mwandishi Wetu
Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliyekuwa akipatiwa matibabu nchini Afrika Kusini amefariki dunia leo..

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Bw. Assaa Rashid leo jioni (Jumanne, Novemba 12, 2013), Dkt. Sendongo Mvungi majira ya saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini akiwa katika Hospitali ya Milpark.

“Kwa masikitiko makubwa, Tume inawafahamisha wananchi kuwa Mjumbe wake, Dkt. Sengondo Mvungi aliyekuwa akipata matibabu katika Hospital ya Milpark iliyopo jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini amefariki dunia leo (Jumanne, Novemba 12, 2013) saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini,” amesema Bw. Rashid katika taarifa yake fupi ya awali na kuongeza:

“Taratibu za kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka nchini Afrika Kusini kuja nchini kwa mazishi zinaendelea na taarifa zaidi zitatolewa kesho (Jumatano, Novemba 13, 2013),” ameongeza.
 

Marehemu Dkt. Mvungi alisafirishwa siku ya Alhamisi, Novemba 7, 2013 kwenda nchini Afrika Kusini kwa uchunguzi na matibabu zaidi akitokea Kitengo cha Mifupa Muhimbili (MOI) aliokuwa amelazwa baada ya kuvamiwa nyumbani kwake Kibamba, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam na watu waliomjeruhi vibaya kichwani usiku wa kuamkia siku ya Jumapili, Novemba 3, 2013.

Katika taarifa yake, Tume pia imewaomba watanzania wote kuungana na familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Dkt. Mvungi katika kuomboleza msiba huo.

Na Omega S. Ngole
Principal Information Officer,
Constitutional Review Commission (Tanzania),
PO Box 1681,
Dar es Salaam,
Tel: +255 (0) 22 2133425,
Fax: +255 (0) 22 2133442,
Mobile: +255 (0) 757 500800,
Website: www.katiba.go.tz
Facebook:www.facebook.com/people/Omega-Ngole
Twitter: https://twitter.com/OmegaNgole

No comments:

Post a Comment