ADVERT 1

ADVERT 1
Kilio na kimbilio la wanahabari Tanzania

Monday, October 1, 2012

WADAU DADA ZETU KATIKA FACEBOOK WAMEANZA KUFUNGUKA KUHUSU MAVAZI YASIO NA HESHIMA

.
Kampeni ya mavazi katika mtandao  wa face book  imeendelea  kuwafungua mabinti wengi ambao baadhi yao  walikuwa ktk ndoto ya kuja kuiga kuvaa vibaya na baadhi  yao wao  walikuwa  wakiona  sawa  kupiga picha za nusu uchi na  kuziweka ktk kurasa  zao za fb .
Kiukweli kwa  siku mbili hizi  kurasa za fb zimeanza  kuvutia kutazamwa na watoto na watu wenye heshima  zao baada ya akina dada wengi kufunguka na kuanza kutokelezea kwa mavazi ya heshima .
pichani ni dada Lily Lulandala ambae yeye ameamua hata kubadili picha yake ktk mwonekano wa ukurasa wake wa fb kutoka ile ya awali ambayo ipo hapo juu ya pili na kutokelezea vingine kwa kuweka picha hii hapa chini ya mwisho .
Mtandao  huu  unaungana na wadau wote  wasiopenda picha za nusu uchi iwe kwa akina  dada na akina kaka  kuwapongeza  waliofunguka na kuvaa kwa heshima  zaidi ombi kwa wadau  wote  waliopo ktk fb na blog kutozipa nafasi picha za nusu uchi ili wanaopenda kupiga picha hizo  waziweke ktk albam zao chumbani kwao

No comments:

Post a Comment