WADAU DADA ZETU KATIKA FACEBOOK WAMEANZA KUFUNGUKA KUHUSU MAVAZI YASIO NA HESHIMA
Kampeni ya mavazi katika mtandao wa face book
imeendelea kuwafungua mabinti wengi ambao baadhi yao walikuwa ktk
ndoto ya kuja kuiga kuvaa vibaya na baadhi yao wao walikuwa wakiona
sawa kupiga picha za nusu uchi na kuziweka ktk kurasa zao za fb .
Kiukweli kwa siku mbili hizi kurasa za fb zimeanza kuvutia kutazamwa
na watoto na watu wenye heshima zao baada ya akina dada wengi kufunguka
na kuanza kutokelezea kwa mavazi ya heshima .
pichani ni dada Lily Lulandala ambae yeye ameamua hata kubadili picha
yake ktk mwonekano wa ukurasa wake wa fb kutoka ile ya awali ambayo ipo
hapo juu ya pili na kutokelezea vingine kwa kuweka picha hii hapa chini
ya mwisho .
Mtandao huu unaungana na wadau wote wasiopenda picha za nusu uchi iwe
kwa akina dada na akina kaka kuwapongeza waliofunguka na kuvaa kwa
heshima zaidi ombi kwa wadau wote waliopo ktk fb na blog kutozipa
nafasi picha za nusu uchi ili wanaopenda kupiga picha hizo waziweke ktk
albam zao chumbani kwao
No comments:
Post a Comment