ADVERT 1

ADVERT 1
Kilio na kimbilio la wanahabari Tanzania

Sunday, October 21, 2012

TUNAIPELEKA WAPI DUNIA , MAKANISA YANAANZISHWA KAMA BAR ZA POMBE ZA KIENYEJI




Shalom!
Wapendwa naomba tusimame katika kuomba huruma ya Mungu na atupe Roho wake Mtakatifu tuogope kabisa kumfanyia Mungu mzaha. Tuko katika wakati mgumu sana nyakati hizi za mwiso, wapo “watumishi wa mungu” wanaohubiri kwa kutumia Maandiko Matakatifu/Biblia lakini nguvu wanazotumia ni za kununua/za giza! Wameusoma upepo uliopo sasa kuwa watu wamejawa na matatizo mengi na tabu nyingi, sasa mahubiri yanayohubiriwa yamebakia kuwa ya upande mmoja tu! MAZURI. Watu wanahubiriwa kupata nyumba, magari, biashara kubwa, watoe/wapande mbegu wapate baraka tele za kusukwa sukwa (mtu kabeba chuki na mtu moyoni mwake miaka hajaachilia) nk. Mambo mengine ya msingi kama kusamehe waliokukosea, kupenda na kuwaombea maadui, kutoa kwa makundi mbalimbali ya wahitaji nk hayaelezwi. Jinsi ya kujenga uhusiano mzuri na Mungu ili kuweza kukabiliana na mitihani ama changamoto mbalimbali za maisha ya ndoa, kazi, imani nk havifundishwi.
Watu wanapatwa na changamoto hizi kwa vile watumishi wa Mungu hawafundishi waumini wao namna ya kukabiliana na mateso mbalimbali kadiri ya maandiko na mifano mbalimbali ya watu walivyoshinda changamoto katika Biblia kwa kumtegemea Mungu. Kwa sababu yakutokufundishwa hayo utakuta watu wana giveup na kuona suluhu ni kuhamahama makanisa kutafuta watakapopata miujiza ama suluhu ya matatizo yao na bado hawapati. Na watu wakipata utajiri ama mazuri wanarudi kumsifu na kumshukuru/kumsifu mtumishi na mtumishi anakuwa “very proud” kwa sifa hizo. Haturudishi Sifa Shukrani na Utukufu kwa Mungu.
Kwa kweli Tunahitaji kuomba, kanisa limeyumba! Halina baba mlezi wa kukemea mambo, sasa kuanzisha makanisa imekuwa kama kuanzisha biashara. Kila leo kanisa jipya na kila mmoja anasema kwake ndiko bora. Hebu tuombe kwa ajili ya wimbi hili wapendwa!

No comments:

Post a Comment