ADVERT 1

ADVERT 1
Kilio na kimbilio la wanahabari Tanzania

Friday, October 19, 2012

Katibu wa Baraza la Jumuiya za Kiislamu Ponda Issa Ponda alikamatwa siku ya Jumanne kwa tuhuma za kuchochea ghasia na kuvunja amani jijini Dar es Salaam, kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Suleiman Kova. Ponda aliitisha maandamano dhidi ya ardhi iliyonunuliwa kutoka Baraza la Waislamu Tanzania na Kampuni ya Agritanza.
Ponda pia anatuhumiwa kuchochea vurugu kufuatia mvulana mmoja kuikojolea Qu'ran mapema wiki hii. Vile vile anatuhumiwa kuchochea maandamano haramu miongoni mwa wafuasi wake juu ya kiwanja kilichouzwa kihalali, lakini anasema lazima kibakie mikononi mwa Waislamu.
Idadi kubwa ya polisi wa Dar es Salaam walipelekwa katika wilaya ya kibiashara katikati ya mji kuwadhibiti waandamanaji waliokerwa na kukamatwa kwa Ponda. Waandamanaji wanne walikamatwa na polisi walitumia gesi za machozi na magari ya maji kutawanya umati wa watu.
Mjini Zanzibar, vijana walitaka kujua taarifa za Sheikh Farid Hadi Ahmed, kiongozi wa Jumuiya ya Maimamu visiwani humo, ambaye alitoweka siku ya Jumanne.
Polisi hawajui alipo na wanachunguza kutoweka kwake, alisema kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa Mjini/Magharibi Said Juma. Aliongeza kwamba vijana wanaoandamana wameziba mitaa kwa mawe, taka na matairi yaliyochomwa moto na wameunguza majengo.

No comments:

Post a Comment