VIFO VYA MAPEMA BARANI AFRIKA! KWA NINI?

Ni nadra kwa kiongozi wa nchi yoyote kufariki akiwa angali madarakani.
Tangu
mwaka 2008, hili limefanyika mara kumi na tatu kote duniani -lakini
kumi kati ya viongozi hao wamekuwa marais wa nchi za afrika.
Kwa nini vifo kama hivi vinatokea sana barani Afrika?
Makundi
makubwa ya watu walikusanyika kushuhudia jeneza la hayati waziri mkuu
wa Ethiopia meles Zenawililipokuwa likipitishwa katikati mwa mji mkuu
Addis Ababa, mnamo siku ya Jumanne wiki iliyopita. Alifariki akiwa na
umri wa miaka 57, baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Mapema
mwezi huu, maelfu ya wananchi wa Ghana walihudhuria mazishi ya hayati
rais, John Atta Mills, aliyefariki ghafla akiwa na umri wa miaka 68.
Miezi
minne kabla ya kifo cha Atta Mills, siku ya kitaifa ilitangazwa nchini
Malawi kuwezesha maelfu ya watu kuhudhuria mazishi ya hayati rais
Bingu wa Mutharika, aliyefariki akiwa na umri wa miaka 78 kutokana na
mshtuko wa moyo.
Na
mnamo mwezi Januari, rais wa Guinea Bissau, Malam Bacai Sanha,
alifariki katika hospitali ya kijeshi mjini paris baada ya kuugua kwa
muda mrefu. Alikuwa na umri wa miaka 64.
Kwa
hivyo viongozi wanne wa Afrika wamefariki mwaka huu pekee . Bila shaka
ni pigo kwa nchi husika na huzuni kubwa kwa familia za viongozi hao.
Lakini je mwandishi wa habari atafsiri vipi matukio haya?
"Kila
usiku Napata simu nyingi kutoka kwa watu wengi kuniambia rais wa
Afrika ameaga dunia" anasemaSimon Allison, mwandishi habari wa mtandao
wa habari wa Daily Maverick nchini Afrika Kusini. "Kwa nini viongozi
wengi wa Afrika wanafariki sana wakati huu? anahoji Simon.
Swali hili bila shaka linasababisha tathmini ya maisha ya viongozi hao.
"
Ukitafakari kidogo orodha ya viongozi wa Afrika waliofariki bila shaka
ni ndefu'' anasemaAllison. Tangu mwaka 2008, viongozi 10 wa Afrika
wamefariki wakiwa madarakani.
Viongozi
wengine wa Afrika waliofariki wakiwa madarakani ni pamoja na Muammar
Gaddafi akiwa na miaka 69. Aliauawa wakati wa mapinduzi ya kiraia nchini
Libya Oktoba mwaka 2011
Aliyekuwa
rais wa Nigeria Umaru Yar'Adua aliaga akiwa na miaka 58 mwezi Mei
mwaka 2010 kutokana na maradhi ya figo pamoja na moyo.
Omar Bongo wa Gabon akiwa na miaka 73 alifariki mwaka 2009
Raia wa Guinea Bissau president, J B Vieira umri wa miaka 69 aliuawa mwezi Machi mwaka 2009
Rais wa Guinea Lansana Conte aliaga akiwa na miaka 74 mwaka 2008, kutokana na sababu zisizojulikana.
Aliyekuwa rais wa Zambia , Levy Mwanawasa akiwa na miaka 59 mwaka 2008, kutokana na kiharusi.
Bila
shaka ni kweli kuwa viongozi wengi wa Afrika wanaaga dunia wakiwa
wangali madarakani kuliko katika bara lengine lolote duniani. Katika
kipindi hicho ni viongozi watatu pekee waliofariki wakiwa wangali
madarakani kwingineko duniani.
Kim
Jong Il wa Korea kaskazini , rais wa Poland, Lech Kaczynski,
aliyefariki katika ajali ya ndege na David Thomson wa Barbados,
aliyefariki kutokana na saratani.
Jibu
la wazi ni kuwa marais wa Afrioka ndio wakongwe zaidi kuliko marais wa
mabara mengine.Tathmini inayotolewa hapa ni kuwa waafrika wanapenda
wenyewe kuwa na viongozi wazee kwani kulingana na utamaduni , wanapata
heshima kubwa kutoka kwa jamii.
Muda
mrefu zaidi ambao marais wa Afrika wanaweza kuishi inakadariwa kuwa
miaka 61 sawa na bara Asia. Viongozi wa bara la Afrika, umri wao
unakakadiriwa kuwa miaka 55 wakati barani Afrika rais mkongwe zaidi
anakadiriwa kuwa na miaka 59.
Lakini
kitu kingine cha kutafakari ni umri mrefu zaidi wanaoishi watu wa bara
hilo ikikadiriwa kuwa chini sana barani Afrika ikilinganishwa na
mabara mengine kama Uropa, Amerika ya kusini na barani Asia.
Sababu
kuu hapa ikiwa ni janga la ukimwi, na pia miundo msingi duni ya afya
ambayo inachangia idadi kubwa ya vifo hasa miongoni mwa watoto
wachanga.
Lakini
umaskini katika maisha ya ujana na kwa watoto wachanga pia zinaathiri
kubwa katika umri wa mtu kulingana na daktari George Leeson wa chuo
kikuu cha Oxford.
"marais
wa Afrika kabla ya kuchaguliwa huenda waliishi maisha ambayo sio
mazuri sana na bila shaka hilo litaathiri maisha yao uzeeni'' anasema
daktari Leeson.
Kwa
hivyo wakati wanapoingia madarakani, licha ya kuwa sasa wanaishi
maisha ya kifahari zaidi kuliko siku zao za utotoni, bado athari za
maisha duni walipokuwa wachanga huwaandama
Lakini
hii haimaanishi kuwa viongozi wote wa Afrika waliishi maisha duni
walipokuwa wadogo. Kuna mambo mengine chungu nzima ya kuzingatia.
Mfano, siasa, dhana kwamba, viongozi wa afrika wanapenda kung'ang'ania
madarakani, hadi watapofariki. Lakini dhana hii ingali kuthibitishwa.
Lakini
kunao viongozi waliong'ang'ania madaraka hadi wakafa, kama vile Omar
Bongo, Conte na Gaddafi, kulingana na tathmini mbali mbali. Lakini
wengine kama Meles Zenawi waligandia tu madarakani , kwa sababu kama
Zenawi, alikuwa na miaka 57 pakee.
Hata hivyo ni muhimu kujua kuwa tathmini hii ni ya viongoiz tu waliofariki wakiwa ofisini tangu mwaka 2008.
SOURCE: BBC
No comments:
Post a Comment