ADVERT 1

ADVERT 1
Kilio na kimbilio la wanahabari Tanzania

Tuesday, September 11, 2012

UN YAPOKEA HILI..............





Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amekaribisha kuchaguliwa Rais Mpya wa Somalia na kuitaja hatua hiyo kuwa ni kumalizika kipindi cha mpito nchini humo. 

Ban Ki Moon ametoa taarifa kwa mnasaba wa kuchaguliwa Rais Mpya wa Somalia Hassan Sheikh Mahmoud na kueleza kuwa Umoja wa Mataifa unalipongeza bunge jipya la Somalia kutokana na uchaguzi huo kufanyika katika mazingira ya utulivu na ya amani. 

Ban Ki Moon amekaribisha kukamilika mchakato wa kipindi cha mpito huko Somalia na kumtaka Rais Hassan Sheikh Mahmoud kuwa na nafasi kuu katika mchakato wa ujenzi mpya na kurejesha uthabiti huko Somalia kwa kuchagua serikali yenye nguvu. 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa aidha ametaka kuendelezwa mashirikiano na misaada ya nchi jirani na Somalia ili kurejesha uthabiti na usalama

No comments:

Post a Comment