Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amekaribisha kuchaguliwa
Rais Mpya wa Somalia na kuitaja hatua hiyo kuwa ni kumalizika kipindi cha mpito
nchini humo.
Ban Ki Moon ametoa taarifa kwa mnasaba wa kuchaguliwa Rais Mpya wa
Somalia Hassan Sheikh Mahmoud na kueleza kuwa Umoja wa Mataifa unalipongeza
bunge jipya la Somalia kutokana na uchaguzi huo kufanyika katika mazingira ya
utulivu na ya amani.
Ban Ki Moon amekaribisha kukamilika mchakato wa kipindi
cha mpito huko Somalia na kumtaka Rais Hassan Sheikh Mahmoud kuwa na nafasi kuu
katika mchakato wa ujenzi mpya na kurejesha uthabiti huko Somalia kwa kuchagua
serikali yenye nguvu.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa aidha ametaka kuendelezwa
mashirikiano na misaada ya nchi jirani na Somalia ili kurejesha uthabiti na usalama
No comments:
Post a Comment