Waziri Kagasheki Awasha Moto katika wizara yake
Waziri
wa Maliasili na Utalii Mhe. Khamis Kagasheki (pichani) amewataka wafanyakazi wa wizara
hiyo kutekeleza wajibu wa kutekeleza kazi kwa
ubunifu na uadilifu huku wakizingatia Sheria, Kanuni na taratibu zinazosimamia
utendaji kazi.
Balozi Kagasheki alitoa rai hiyo
wakati akifungua rasmi mkutano wa 20 wa Baraza la
Wafanyakazi la Wizara ya Maliasili na Utalii uliofanyika jijini Dar es Salam.
Mhe. Waziri aliwataka wajumbe wa
wajumbe wa baraza hilo kutambua kuwa Baraza ni chombo muhimu kwa ajili ya
kuongeza ufanisi na tija katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara.
“Tumieni vema nafasi mlizonazo kuhakikisha kuwa haki na
wajibu wa Mwajiri na Mtumishi vinapewa kipaumbele katika utekelezaji wa
majukumu yenu kwa kulinga maslahi ya pande zote mbili kwa manufaa ya Taifa
zima.
“Moja ya changamoto mliyonayo kama Baraza hili ni
kuhakikisha watumishi wanazingatia nidhamu na maadili katika utumishi wa
umma.
Ninafahamu mazingira ya kazi na
hasa katika vituo vyetu si ya kuridhisha, lakini ni vyema tukahimiza watumishi
kufuata kikamilifu Sheria, Kanuni na taratibu za utendaji wa kazi”, anasema
Kagasheki.
Anasema wajumbe wakitekeleza wajibu wao kama Wajumbe wa Baraza, watarahisisha kazi ya
utekelezaji wa majukumu ya Wizara.