ADVERT 1

ADVERT 1
Kilio na kimbilio la wanahabari Tanzania

Monday, November 12, 2012

Uchafu ndani ya Manispaa ya Iringa wazidi

Chomo cha kuhifadhi takataka kikiwa barabarani maeneo ya msikitini Kihesa.
Ikiwa viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa wakiueleza umma kuwa wanawajibika katika suala la usafi, hali ya usafi bado inadorora.

Licha ya kuweka baadhi ya vifaa vya kuhifadhia takataka maarufu kwa jina la madampo, yamekuwa yakikaa kwa muda mrefu bila kuhamishwa kwenda kumwaga uchafu huo na kusababisha usumbufu kwa wananchi wa maeneo yanayolizunguka dampo husika.

Moja ya dampo ambalo kila wakati husahauli kubwebwa kwenda kutupwa uchafu huo ni lle ambalo lipo maeneo ya msikitini Kihesa ambalo huutumiwa na kila mtu wakiwemo wapitanjia.

Licha ya kusahaulika, dampo hilo liko barabarani hali inayoweza kusababisha ajali wakati wowote kwa wananchi wanaotembea kwa miguu au magari wakati wa kupishana.

Mtandao huu ulimkariri Meya wa Manispaa ya Iringa Amani Mwamwindi alikisema kuwa hali ya usafi katika Manispaa inaridhisha kwani wamejipanga vizuri kwa ajili ya usafi.

Pamoja na kujidai kuwa halmashauri imejipanga vizuri kwa ajili ya usafi, Mwamwindi kila wakati amekuwa akilalamika kuwa Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mch. Peter Msigwa amewaachia kazi hiyo.

Kwa upande wake Mch. Msigwa alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari alisema kuwa, kazi ya usafi katika Manispaa mipango yote inatakiwa kufanywa na Meya kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Halmashauri.(Story from www.GUSTAV CHAHE.blogsport.com)

WAKALI WA MIC, TWANGA PEPETA, WAFUNIKA DAR LIVE


Washiriki wote wakiwa pamoja kabla ya kuanza shindano hilo.
Mmoja wa washiriki akionyesha hazina yake katika sanaa hiyo.
Washindi  wa tano bora.
Luiza Mbutu (kushoto) wa Twanga Pepeta akiimba na mwanamuziki mwenzake.
Wanenguaji wa Twanga Pepeta wakiwa kazini.
Majaji Ally Baucha, (kulia) John Dilinga na Abdalah Mrisho (kushoto) wakifuatilia shindano hilo.
Mshiriki akikamua kwa madoido.
Kinadada wakifuatilia shindano hilo.
Mashabiki wa soka wakifuatilia mpambano kati ya Chelsea na Liverpool ukumbini humo.
SHINDANO la kumtafuta mkali wa ‘maiki’, The Mic King,  lililoendelea na kufanyika jana  Jumapili  katika ukumbi wa kisasa wa burudani wa Dar Live ulioko Mbagala jijini Dar es Salaam,  na kusindikizwa na Bendi ya African Star ‘Twanga Pepeta’,  lilitoa burdani ya aina yake kutokana na vijana washiriki kutoka wilayani Temeke kuonyesha umahiri mkubwa katika muziki wa kufokafoka.
Story by www.francisgodwin.blogspot.com