Uchafu ndani ya Manispaa ya Iringa wazidi
Chomo cha kuhifadhi takataka kikiwa barabarani maeneo ya msikitini Kihesa. |
Licha ya kuweka baadhi ya vifaa vya kuhifadhia takataka maarufu kwa jina la madampo, yamekuwa yakikaa kwa muda mrefu bila kuhamishwa kwenda kumwaga uchafu huo na kusababisha usumbufu kwa wananchi wa maeneo yanayolizunguka dampo husika.
Moja ya dampo ambalo kila wakati husahauli kubwebwa kwenda kutupwa uchafu huo ni lle ambalo lipo maeneo ya msikitini Kihesa ambalo huutumiwa na kila mtu wakiwemo wapitanjia.
Licha ya kusahaulika, dampo hilo liko barabarani hali inayoweza kusababisha ajali wakati wowote kwa wananchi wanaotembea kwa miguu au magari wakati wa kupishana.
Mtandao huu ulimkariri Meya wa Manispaa ya Iringa Amani Mwamwindi alikisema kuwa hali ya usafi katika Manispaa inaridhisha kwani wamejipanga vizuri kwa ajili ya usafi.
Pamoja na kujidai kuwa halmashauri imejipanga vizuri kwa ajili ya usafi, Mwamwindi kila wakati amekuwa akilalamika kuwa Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mch. Peter Msigwa amewaachia kazi hiyo.
Kwa upande wake Mch. Msigwa alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari alisema kuwa, kazi ya usafi katika Manispaa mipango yote inatakiwa kufanywa na Meya kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Halmashauri.(Story from www.GUSTAV CHAHE.blogsport.com)